Polisi wakamata washukiwa 56 wa vurugu Kuresoi North

Maafisa wa polisi wamewakamata washukiwa 56 wanaohusishwa na vurugu zilizoshuhudiwa Ijumaa katika eneo la Kuresoi North, kaunti ya Nakuru. Polisi wamesema wanaendelea kuwatafuta watu wengine wanaohusishwa na tukio hilo, akiwemo Mbunge wa Kuresoi North Alfred Mutai, kuhusiana na vurugu hizo zilizosababisha majeruhi watatu. Polisi wamesema vurugu hizo zilihusishwa na makundi ya wahuni wanaodaiwa kufadhiliwa na baadhi ya wanasiasa, na zilijiri wakati wa mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Gavana wa Nakuru Susan Kihika katika eneo hilo. Ben Kirui anaripoti zaidi.