Uzushi wa Maulidi 🎙Sheikh: Nassor Bachu {Rahimahullāh}]

HISTORIA YA MAULIDI. Yeyote mwenye kutazama maisha ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na historia ya Maswahaba zake (Radhwiya Allaahu ‘anhum), Taabi‘iyna na waliowafuata kwa wema mpaka kufikia zaidi ya mwaka wa 350 Hijri hatumuoni hata mwanachuoni mmoja wala mahakimu (viongozi) na wala watu wa kawaida waliokuwa wakifanya mawlid au wakaamrisha au wakahimiza au wakazungumza juu yake. Amesema al-Haafidhw as-Sakhawiy: “Shughuli za kufanya Mawlid matukufu hayakupokelewa na watangu wema (Salafus Swaalih) wa karne tatu bora za mwanzo. Kwa hakika jambo hili lilizuliwa baada yake.” [Imenukuliwa kutoka kwaSubulul Hudaa war Rashaad cha As-Salihiy, Mj. 1, uk. 439].   Suala la sisi kujiuliza ni kuwa; Je, haya Mawlid yalianza lini? Jawabu ya suala hili kwa mwanachuoni wa Ki-Sunnah, Al-Imaam al-Maqriyziy: “Katika kipindi cha uongozi wa Faatwimiyyuun (hawa walikuwa ni Rawaafidh (Mashia) katika kipote cha Ismailiyyah [Makoja] katika nchi ya Misri) walikuwa wanachukuwa hii ni misimu ya sherehe ambapo walikuwa wakiwakunjulia hali za raia zao na kuwakithirishia neema. Na walikuwa hawa watawala wa Faatwimiyyuun katika mwaka mzima wana misimu ya sherehe na Idi zao nazo ni kama zifuatazo: Msimu wa kichwa cha mwaka, Msimu wa mwanzo wa mwaka, Sherehe za ‘Aashuraa, na Mawlid ya Nabii (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), na Mawlid ya ‘Aliy bin Abi Twaalib (Radhwiya Allaahu ‘anhu), na Mawlid ya Hasan na Husayn (Radhwiya Allaahu ‘anhuma), na Mawlid ya Faatwimah az-Zahraa (Radhwiya Allaahu ‘anha), na Mawlid ya kiongozi wao aliye hai kwa wakati ule, usiku wa kwanza wa Rajab, na usiku wa kati ya Rajab, na Mawlid ya usiku wa Ramadhaan na mwisho wa Ramadhaan na Msimu wa 'Iydul Fitwr na Msimu wa 'Iydul Adh-ha na Idi ya Ghaadir, Msimu wa ufunguzi wa Ghuba na Siku ya Nairuuz na Siku ya Ghatas na Siku ya Mazazi, na Siku ya Vipandio, Kis-wa (nguo) ya Msimu wa Kusi na Kaskazi, Alhamisi ya Adasi na Siku ya Ubatizo.” [Al-Khutwat, Mj. 1, uk. 490 na baada yake].  na amesema tena katika kitabu chengine: “Na katika mwezi wa Rabi’ul Awwal walijilazimisha watu kuwasha kandili usiku katika njia zote na vichochoro vyake huko Misri.” Na amesema tena al-Maqriiziy katika maudhui nyengine: “Shughuli za Mawlid ya Mtume mtukufu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) zilikuwa zikifanyika rasmi kama desturi yake katika mwezi wa Rabi’ul Awwal.” Kila mmoja anatakiwa azingatie jinsi gani Mawlid yalivyoanzishwa pamoja na uzushi mkubwa mfano: Uzushi wa kukataa na kuchupa mipaka juu ya familia ya Mtume kwa kusimamisha mawlid ya ‘Aliy, Faatwimah, Hasan na Husayn.   Uzushi wa kusherehekea Idi ya Nayruuz, na Idi ya Ghatas na kuzaliwa kwa Masihi nazo ni Idi za Wakristo. Amesema Ibn Turkumani kuhusu hizi Idi za Wakristo: “Na miongoni mwa uzushi inayoleta hizaya ni wanaofanya Waislamu katika siku ya Nayruuz ya Kikristo na misimu yao mengine na siku kuu ('Iyd) kwa kupeana chakula kwa wingi. Na sadaka ya chakula isiyokubalika itarudi kwa mwenye kutoa kwa haraka au baadae. Na kwa uchache wa tawfiki na kufaulu ni yale wanayofanya Waislamu waovu kwa inayotambuliwa kama siku ya mazazi (yaani kuzaliwa kwa 'Iysaaa).” [Al-Lam‘i Fil Hawaadith wal Bid’ah, Mj. 1, uk. 293 – 316]. Na imenukuliwa kutoka kwa Wanachuoni wa Hanafiyyah kwamba yeyote ambaye atafanya mambo yaliyotangulia atakuwa kafiri mfano wao (hao Wakristo). Na wakataja idadi za Idi kadhaa za Wakristo ambao Waislamu walio wajinga wanashiriki, na jinsi zilivyo uharamu wake katika Kitabu na Sunnah na yale misingi ya kishariy'ah yaliyo kamili.   Watu wa kwanza kuzua kile kinachoitwa Mawlid ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ni Bani ‘Ubayd ambao walikuwa wakijulikana kama Faatwimiyyuun. Haya yametajwa na Wanachuoni wengi mfano Mufti wa Misri wa zamani, Shaykh Muhammad Bakhiit al-Mutii‘y katika kitabu chake Ahsanul Kalaam Fi maa Yata‘alaq Bis Sunnah wal Bid‘ah Minal Ahkaam; Shaykh ‘Aliy Mahfuudh katika kitabu chakeAl-Ibda‘ Fiy Madh-har al-Ibtidaa‘; Shaykh Isma‘iyl al-Answaariy katika kitabu chakeAl-Qawlul Fasl Fiy Hukmil Ihtifaal Bi Mawlid Khayrir Rasuul

MSAMAHA WA KWELI KWA ALLAH - SHEIKH NASSOR BACHU
▶︎

MSAMAHA WA KWELI KWA ALLAH - SHEIKH NASSOR BACHU

Umuhimu Wa Adhkar {Sheikh Nassor Bachu {Rahimahullāh}]
▶︎

Umuhimu Wa Adhkar {Sheikh Nassor Bachu {Rahimahullāh}]

𝗞𝗔𝗨𝗟𝗜 𝗡𝗭𝗜𝗧𝗢 𝗔𝗟𝗜𝗭𝗢𝗪𝗔𝗛𝗜 𝗞𝗨𝗭𝗜𝗧𝗔𝗠𝗞𝗔 𝗦𝗛𝗘𝗜𝗞𝗛 𝗡𝗔𝗦𝗦𝗢𝗥 𝗕𝗔𝗖𝗛𝗨 رحمه الله
▶︎

𝗞𝗔𝗨𝗟𝗜 𝗡𝗭𝗜𝗧𝗢 𝗔𝗟𝗜𝗭𝗢𝗪𝗔𝗛𝗜 𝗞𝗨𝗭𝗜𝗧𝗔𝗠𝗞𝗔 𝗦𝗛𝗘𝗜𝗞𝗛 𝗡𝗔𝗦𝗦𝗢𝗥 𝗕𝗔𝗖𝗛𝗨 رحمه الله

Siku ya malipo||Sheikh Nassor Bachu 1988.
▶︎

Siku ya malipo||Sheikh Nassor Bachu 1988.

HISTORIA YA BANII ISRAIL part 1
▶︎

HISTORIA YA BANII ISRAIL part 1

SHK MSELEM MTUME MUHAMMAD AMESIFIWA MPAKA KWENYE MAULIDI | KUINGIYA KATIKA UISLAMU HAKUNA TOZO BURE
▶︎

SHK MSELEM MTUME MUHAMMAD AMESIFIWA MPAKA KWENYE MAULIDI | KUINGIYA KATIKA UISLAMU HAKUNA TOZO BURE

Kukataza Mambo Ya Bid'ah. [Sheikh Nassor Bachu Rahimahullāh]
▶︎

Kukataza Mambo Ya Bid'ah. [Sheikh Nassor Bachu Rahimahullāh]

shekh Nassor bachu akitoa mawaidha mwaka wa huzun wa mtume muhammad (s.w.s)
▶︎

shekh Nassor bachu akitoa mawaidha mwaka wa huzun wa mtume muhammad (s.w.s)

shekh Nassor bachu akitoa mawaidha kuhusu subra na mafanikio y uhakika part1 lengo kupata mazingatio
▶︎

shekh Nassor bachu akitoa mawaidha kuhusu subra na mafanikio y uhakika part1 lengo kupata mazingatio

KUMSOMEA MGONJWA SURATUL YASSIN

[SHEIKH  NASSOR BACHU {RAHIMAHULLAH}]
▶︎

KUMSOMEA MGONJWA SURATUL YASSIN [SHEIKH NASSOR BACHU {RAHIMAHULLAH}]

MATUKIO YA SIKU YA MALIPO 2/2 - SHEIKH NASSOR BACHU
▶︎

MATUKIO YA SIKU YA MALIPO 2/2 - SHEIKH NASSOR BACHU

KISA CHA IMAM MALIK BIN ANAS  SH NASSOR BACHU
▶︎

KISA CHA IMAM MALIK BIN ANAS SH NASSOR BACHU

MAMBO YALIYOZULIWA KWENYE MAZISHI 4/7 - SHEIKH NASSOR BACHU
▶︎

MAMBO YALIYOZULIWA KWENYE MAZISHI 4/7 - SHEIKH NASSOR BACHU

ZIJUE LADHA TISINI NA TISA ANAZOZIPATA MWANAMKE KATIKA TENDO LA NDOA. SHEKH NASSORO BACHU.
▶︎

ZIJUE LADHA TISINI NA TISA ANAZOZIPATA MWANAMKE KATIKA TENDO LA NDOA. SHEKH NASSORO BACHU.

Kisa cha Nabii Ayub (Alayhi salam)  - Sheikh Nassor Bachu
▶︎

Kisa cha Nabii Ayub (Alayhi salam) - Sheikh Nassor Bachu

Othman Maalim - Hukmu ya Kusoma Maulid
▶︎

Othman Maalim - Hukmu ya Kusoma Maulid

TAJIRI: SHEIKH NASSOR BACHU
▶︎

TAJIRI: SHEIKH NASSOR BACHU

Je Kusherehekea Maulidi ni Kheri? - Dr Muhammad Islam Salim
▶︎

Je Kusherehekea Maulidi ni Kheri? - Dr Muhammad Islam Salim

IKIWA NI MWANAUME HILI LINAKUHUSU / WANAWAKE - SH NASSOR BACHU
▶︎

IKIWA NI MWANAUME HILI LINAKUHUSU / WANAWAKE - SH NASSOR BACHU

MAMBO HAYA AKIWANAYO MTU ANAKUWA NA KIBRI MBELE YA ALLAH SHEIKH NASSOR BACHU
▶︎

MAMBO HAYA AKIWANAYO MTU ANAKUWA NA KIBRI MBELE YA ALLAH SHEIKH NASSOR BACHU