Nakuru: Kilio cha penzi kwa mke

Kwa wengi ambao hufunga ndoa, ahadi ya kupendana wakati wa shida na raha, huwa haina maana kuu hadi pale msiba na changamoto vitabisha hodi. Katika kaunti ya Nakuru kuna familia moja ambayo imestahimili mengi kwa sababu ya maradhi ya kisukari yanayomhangaisha Grace Mburu. Mumewe Grace, James Mburu anasema kuwa wameweza kustahimili yote kwa sababu ya mapenzi. Grace amekuwa mdhaifu kwa ugonjwa kwa takriban mwaka mmoja sasa na hawezi kuendesha shughuli za kawaida, ila Mburu ameamua ‘kufa naye’.