Ol Kalou yafufua kumbukumbu za uchaguzi wa 1995

Kaunti ya Nyandarua imeendelea kuonyesha mwelekeo wake wa kipekee kisiasa, huku matokeo ya uchaguzi mdogo wa Ol Kalou yakifufua kumbukumbu za uchaguzi wa mwaka 1995 katika eneo bunge la Kipipiri. Kuanzia makabiliano kati ya KANU na DP mwaka 1995 hadi ushindani kati ya UDA na DCP mwaka 2026, matukio ya kisiasa yanaonyesha kuwa juhudi za chama tawala kutwaa ngome za upinzani zimeendelea kukumbana na upinzani mkali hata baada ya zaidi ya miaka 30.